16. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18. BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha;Akageuzia mbali naye hasira yake.
19. Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya;Wala usiwahusudu wabaya;
20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.
21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;
22. Maana msiba wao utatokea kwa ghafula;Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.
23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.
24. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki;Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.
25. Bali kwao wakemeao furaha itakuwako;Na baraka ya kufanikiwa itawajilia.
26. Aibusu midomo atoaye jawabu la haki.
27. Tengeneza kazi yako huko nje,Jifanyizie kazi yako tayari shambani,Ukiisha, jenga nyumba yako.