Mit. 24:15-23 Swahili Union Version (SUV)

15. Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki;Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;

16. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18. BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha;Akageuzia mbali naye hasira yake.

19. Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya;Wala usiwahusudu wabaya;

20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.

21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

22. Maana msiba wao utatokea kwa ghafula;Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.

23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.

Mit. 24