13. Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema,Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.
14. Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako;Ikiwa umekwisha kuiona;Ndipo itakapofuata thawabu;Wala tumaini lako halitabatilika.
15. Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki;Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;
16. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;