10. Ukizimia siku ya taabu,Nguvu zako ni chache.
11. Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe;Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.
12. Ukisema, Sisi hatukujua hayo;Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye?Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye?Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?
13. Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema,Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.
14. Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako;Ikiwa umekwisha kuiona;Ndipo itakapofuata thawabu;Wala tumaini lako halitabatilika.
15. Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki;Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;
16. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18. BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha;Akageuzia mbali naye hasira yake.
19. Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya;Wala usiwahusudu wabaya;