Mit. 23:8-17 Swahili Union Version (SUV)

8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.

9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.

10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;

11. Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu;Atawatetea juu yako.

12. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho;Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.

13. Usimnyime mtoto wako mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14. Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.

15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;

16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.

17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;

Mit. 23