Mit. 23:6-22 Swahili Union Version (SUV)

6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.

9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.

10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;

11. Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu;Atawatetea juu yako.

12. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho;Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.

13. Usimnyime mtoto wako mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14. Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.

15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;

16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.

17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;

18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.

19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.

20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.

21. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini,Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.

22. Msikilize baba yako aliyekuzaa,Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.

Mit. 23