4. Usijitaabishe ili kupata utajiri;Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.
5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.
6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;
7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.
9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.
10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;
11. Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu;Atawatetea juu yako.
12. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho;Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.
13. Usimnyime mtoto wako mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14. Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.
15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;
16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.
17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;
18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.
19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.
20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini,Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.