Mit. 23:3-20 Swahili Union Version (SUV)

3. Usivitamani vyakula vyake vya anasa;Kwa maana ni vyakula vya hila.

4. Usijitaabishe ili kupata utajiri;Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.

5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.

6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.

9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.

10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;

11. Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu;Atawatetea juu yako.

12. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho;Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.

13. Usimnyime mtoto wako mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14. Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.

15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;

16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.

17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;

18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.

19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.

20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.

Mit. 23