2. Tena ujitie kisu kooni,Kama ukiwa mlafi.
3. Usivitamani vyakula vyake vya anasa;Kwa maana ni vyakula vya hila.
4. Usijitaabishe ili kupata utajiri;Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.
5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.
6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;
7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.
9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.
10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;