Mit. 23:12-20 Swahili Union Version (SUV)

12. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho;Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.

13. Usimnyime mtoto wako mapigo;Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14. Utampiga kwa fimbo,Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.

15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;

16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.

17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;

18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.

19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.

20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.

Mit. 23