Mit. 23:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala,Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

2. Tena ujitie kisu kooni,Kama ukiwa mlafi.

3. Usivitamani vyakula vyake vya anasa;Kwa maana ni vyakula vya hila.

4. Usijitaabishe ili kupata utajiri;Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.

5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.

6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

Mit. 23