Mit. 23:1-11 Swahili Union Version (SUV)

1. Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala,Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

2. Tena ujitie kisu kooni,Kama ukiwa mlafi.

3. Usivitamani vyakula vyake vya anasa;Kwa maana ni vyakula vya hila.

4. Usijitaabishe ili kupata utajiri;Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.

5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.

6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.

9. Usiseme masikioni mwa mpumbavu;Maana atadharau hekima ya maneno yako.

10. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani;Wala usiingie katika mashamba ya yatima;

11. Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu;Atawatetea juu yako.

Mit. 23