Mit. 22:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.

9. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.

10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.

11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.

12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.

Mit. 22