8. Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.
9. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.
10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.
11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.
12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.