Mit. 22:7-20 Swahili Union Version (SUV)

7. Tajiri humtawala maskini,Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.

8. Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.

9. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.

10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.

11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.

12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko nje;Nitauawa katika njia kuu.

14. Kinywa cha malaya ni shimo refu;Anayechukiwa na BWANA atatumbukia ndani yake.

15. Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto;Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

16. Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato,Naye ampaye tajiri, hupata hasara.

17. Tega sikio lako uyasikie maneno ya wenye hekima, na kuuelekeza moyo wako kwa maarifa yangu;

18. maana ni vizuri kuyahifadhi ndani yako, hali yakithibitika pamoja midomoni mwako.

19. Ili matumaini yako uyaweke kwa BWANA, leo nimekujulisha wewe haya, naam, wewe.

20. Je! Sikukuandikia mambo makuu juu ya mashauri na juu ya maarifa;

Mit. 22