Mit. 22:5-14 Swahili Union Version (SUV)

5. Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu;Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.

6. Mlee mtoto katika njia impasayo,Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

7. Tajiri humtawala maskini,Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.

8. Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.

9. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.

10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.

11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.

12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko nje;Nitauawa katika njia kuu.

14. Kinywa cha malaya ni shimo refu;Anayechukiwa na BWANA atatumbukia ndani yake.

Mit. 22