Mit. 22:22-25 Swahili Union Version (SUV)

22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;

23. Kwa sababu BWANA atawatetea;Naye atawateka uhai wao waliowateka.

24. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi;Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;

25. Usije ukajifunza njia zake;Na kujipatia nafsi yako mtego.

Mit. 22