22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;
23. Kwa sababu BWANA atawatetea;Naye atawateka uhai wao waliowateka.
24. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi;Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;
25. Usije ukajifunza njia zake;Na kujipatia nafsi yako mtego.