21. ili kukujulisha hakika ya maneno ya kweli, uwarudishie wakutumao maneno ya kweli?
22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;
23. Kwa sababu BWANA atawatetea;Naye atawateka uhai wao waliowateka.
24. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi;Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;
25. Usije ukajifunza njia zake;Na kujipatia nafsi yako mtego.
26. Usiwe mmoja wao wawekao rehani;Au walio wadhamini kwa deni za watu;
27. Kama huna kitu cha kulipa;Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?
28. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani,Uliowekwa na baba zako.