Mit. 22:21-28 Swahili Union Version (SUV)

21. ili kukujulisha hakika ya maneno ya kweli, uwarudishie wakutumao maneno ya kweli?

22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;

23. Kwa sababu BWANA atawatetea;Naye atawateka uhai wao waliowateka.

24. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi;Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;

25. Usije ukajifunza njia zake;Na kujipatia nafsi yako mtego.

26. Usiwe mmoja wao wawekao rehani;Au walio wadhamini kwa deni za watu;

27. Kama huna kitu cha kulipa;Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako?

28. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani,Uliowekwa na baba zako.

Mit. 22