2. Tajiri na maskini hukutana pamoja;BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.
3. Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha;Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.
4. Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANANi utajiri, na heshima, nayo ni uzima.
5. Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu;Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo.
6. Mlee mtoto katika njia impasayo,Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
7. Tajiri humtawala maskini,Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
8. Yeye apandaye uovu atavuna msiba,Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma.
9. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa;Maana huwapa maskini chakula chake.
10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.
11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.
12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.