Mit. 22:10-16 Swahili Union Version (SUV)

10. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka;Naam, fitina na fedheha zitakoma.

11. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo;Mfalme atakuwa rafiki yake.

12. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa;Bali huyapindua maneno ya mtu haini.

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko nje;Nitauawa katika njia kuu.

14. Kinywa cha malaya ni shimo refu;Anayechukiwa na BWANA atatumbukia ndani yake.

15. Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto;Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

16. Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato,Naye ampaye tajiri, hupata hasara.

Mit. 22