3. Kutenda haki na hukumuHumpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.
4. Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari,Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
5. Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu;Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.
6. Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongoNi moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
7. Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali;Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.