Mit. 21:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Kutenda haki na hukumuHumpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

4. Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari,Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.

5. Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu;Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

6. Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongoNi moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.

7. Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali;Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.

Mit. 21