Mit. 21:22-30 Swahili Union Version (SUV)

22. Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu;Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.

23. Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake,Atajilinda nafsi yake na taabu.

24. Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi;Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.

25. Matakwa yake mtu mvivu humfisha,Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.

26. Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa;Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.

27. Sadaka ya wasio haki ni chukizo;Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!

28. Shahidi wa uongo atapotea;Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.

29. Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu;Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.

30. Hapana hekima, wala ufahamu,Wala shauri, juu ya BWANA.

Mit. 21