21. Aandamaye haki na fadhili,Ataona uhai na haki na heshima.
22. Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu;Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.
23. Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake,Atajilinda nafsi yake na taabu.
24. Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi;Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.
25. Matakwa yake mtu mvivu humfisha,Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26. Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa;Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.