Mit. 21:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Mtu aikosaye njia ya busaraAtakaa katika mkutano wao waliokufa.

17. Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.

18. Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki;Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.

19. Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika;Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.

20. Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima;Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

Mit. 21