12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.
13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.
14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.
15. Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu;Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.