Mit. 21:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.

13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.

14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.

15. Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu;Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.

Mit. 21