Mit. 21:11-18 Swahili Union Version (SUV)

11. Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima;Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.

12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.

13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.

14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.

15. Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu;Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.

16. Mtu aikosaye njia ya busaraAtakaa katika mkutano wao waliokufa.

17. Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.

18. Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki;Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.

Mit. 21