Mit. 21:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA;Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.

2. Kila njia ya mtu ni sawa machoni pake mwenyewe;Bali BWANA huipima mioyo.

3. Kutenda haki na hukumuHumpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

4. Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari,Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.

5. Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu;Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

6. Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongoNi moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.

7. Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali;Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.

8. Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana;Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.

9. Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini,Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.

Mit. 21