Mit. 20:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu;Nimetakasika dhambi yangu?

10. Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali,Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.

11. Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.

12. Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.

Mit. 20