7. Mwenye haki aendaye katika unyofu wake,Watoto wake wabarikiwa baada yake.
8. Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu,Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
9. Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu;Nimetakasika dhambi yangu?
10. Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali,Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.
11. Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
12. Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.
19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
20. Amlaaniye babaye au mamaye,Taa yake itazimika katika giza kuu.
21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.
22. Usiseme, Mimi nitalipa mabaya;Mngojee BWANA, naye atakuokoa.
23. Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA;Tena mizani ya hila si njema.
24. Mwenendo wa mtu watoka kwa BWANA;Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?
25. Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu;Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.
26. Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki;Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.