26. Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki;Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.
27. Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA;Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.
28. Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme,Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.
29. Fahari ya vijana ni nguvu zao,Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.