Mit. 20:21-29 Swahili Union Version (SUV)

21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.

22. Usiseme, Mimi nitalipa mabaya;Mngojee BWANA, naye atakuokoa.

23. Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA;Tena mizani ya hila si njema.

24. Mwenendo wa mtu watoka kwa BWANA;Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?

25. Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu;Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.

26. Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki;Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.

27. Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA;Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.

28. Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme,Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.

29. Fahari ya vijana ni nguvu zao,Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.

Mit. 20