17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.
19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
20. Amlaaniye babaye au mamaye,Taa yake itazimika katika giza kuu.
21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.
22. Usiseme, Mimi nitalipa mabaya;Mngojee BWANA, naye atakuokoa.
23. Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA;Tena mizani ya hila si njema.
24. Mwenendo wa mtu watoka kwa BWANA;Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?
25. Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu;Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.
26. Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki;Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.
27. Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA;Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.