16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.
19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.