Mit. 20:11-19 Swahili Union Version (SUV)

11. Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.

12. Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.

15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.

16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.

17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.

18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.

19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.

Mit. 20