Mit. 20:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi;Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.

2. Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba;Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.

3. Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake;Bali kila mpumbavu ataka kugombana.

4. Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi;Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.

5. Mashauri ya moyoni ni kama kilindi;Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.

Mit. 20