1. Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi;Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
2. Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba;Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.
3. Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake;Bali kila mpumbavu ataka kugombana.
4. Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi;Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
5. Mashauri ya moyoni ni kama kilindi;Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.