6. Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima;Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;
7. Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili;Yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu;
8. Apate kuyalinda mapito ya hukumu,Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.
9. Ndipo utakapofahamu haki na hukumu,Na adili, na kila njia njema.
10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;
11. Busara itakulinda;Ufahamu utakuhifadhi.
12. Ili kukuokoa na njia ya uovu,Na watu wanenao yaliyopotoka;
13. Watu waziachao njia za unyofu,Ili kuziendea njia za giza;
14. Wafurahio kutenda mabaya;Wapendezwao na upotoe wa waovu;
15. Waliopotoka katika njia zao;Walio wakaidi katika mapito yao.
16. Ili kuokoka na malaya,Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;