3. Naam, ukiita busara,Na kupaza sauti yako upate ufahamu;
4. Ukiutafuta kama fedha,Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;
5. Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA,Na kupata kumjua Mungu.
6. Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima;Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;
7. Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili;Yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu;
8. Apate kuyalinda mapito ya hukumu,Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.