Mit. 2:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Naam, ukiita busara,Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4. Ukiutafuta kama fedha,Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5. Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA,Na kupata kumjua Mungu.

6. Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima;Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;

7. Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili;Yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu;

8. Apate kuyalinda mapito ya hukumu,Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.

Mit. 2