Mit. 2:15-21 Swahili Union Version (SUV)

15. Waliopotoka katika njia zao;Walio wakaidi katika mapito yao.

16. Ili kuokoka na malaya,Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;

17. Amwachaye rafiki wa ujana wake,Na kulisahau agano la Mungu wake.

18. Maana nyumba yake inaelekea mauti,Na mapito yake yanakwenda kwenye wafu.

19. Katika hao wamwendeao harudi hata mmoja,Wala hawazifikilii njia za uzima.

20. Ili upate kwenda katika njia ya watu wema,Na kuyashika mapito ya wenye haki.

21. Maana wanyofu watakaa katika nchi,Na wakamilifu watadumu ndani yake.

Mit. 2