Mit. 19:7-13 Swahili Union Version (SUV)

7. Ndugu zote wa maskini humchukia;Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye!Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.

8. Apataye hekima hujipenda nafsi yake;Ashikaye ufahamu atapata mema.

9. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Naye asemaye uongo ataangamia.

10. Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu;Sembuse mtumwa awatawale wakuu.

11. Busara ya mtu huiahirisha hasira yake;Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;Bali hisani yake kama umande juu ya majani.

13. Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye;Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

Mit. 19