7. Ndugu zote wa maskini humchukia;Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye!Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.
8. Apataye hekima hujipenda nafsi yake;Ashikaye ufahamu atapata mema.
9. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Naye asemaye uongo ataangamia.
10. Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu;Sembuse mtumwa awatawale wakuu.