23. Kumcha BWANA huelekea uhai;Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.
24. Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini;Ila hataki hata kuupeleka kinywani pake.
25. Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara;Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.
26. Apotezaye mali za babaye na kumfukuza mamaye,Ni mwana aaibishaye, na kuleta lawama.
27. Mwanangu, acha kusikia mafundisho,Ukitaka tu kuyaasi maneno ya maarifa.