Mit. 19:16-19 Swahili Union Version (SUV)

16. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake;Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.

17. Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA;Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini;Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.

19. Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake,Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.

Mit. 19