Mit. 19:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Busara ya mtu huiahirisha hasira yake;Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;Bali hisani yake kama umande juu ya majani.

13. Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye;Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye;Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na BWANA.

15. Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;Na nafsi yake mvivu itaona njaa.

16. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake;Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.

Mit. 19