Mit. 19:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.

2. Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa;Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

3. Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake;Na moyo wake hununa juu ya BWANA.

4. Utajiri huongeza rafiki wengi;Bali maskini hutengwa na rafiki yake.

5. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Wala asemaye uongo hataokoka.

6. Watu wengi watamsihi mkuu ili awafadhili;Na kila mtu ni rafiki yake atoaye tunu.

7. Ndugu zote wa maskini humchukia;Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye!Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.

8. Apataye hekima hujipenda nafsi yake;Ashikaye ufahamu atapata mema.

9. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Naye asemaye uongo ataangamia.

Mit. 19