Mit. 19:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.

2. Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa;Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

3. Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake;Na moyo wake hununa juu ya BWANA.

Mit. 19