1. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
2. Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa;Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.
3. Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake;Na moyo wake hununa juu ya BWANA.