9. Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,Ni ndugu yake aliye mharabu.
10. Jina la BWANA ni ngome imara;Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
11. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
12. Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
13. Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.
14. Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
15. Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
16. Zawadi ya mtu humpatia nafasi;Humleta mbele ya watu wakuu.
17. Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
18. Kura hukomesha mashindano;Hukata maneno ya wakuu.
19. Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
20. Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.
21. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;Na wao waupendao watakula matunda yake.
22. Apataye mke apata kitu chema;Naye ajipatia kibali kwa BWANA.
23. Maskini hutumia maombi;Bali tajiri hujibu kwa ukali.