8. Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo;Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
9. Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,Ni ndugu yake aliye mharabu.
10. Jina la BWANA ni ngome imara;Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
11. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.