Mit. 18:19-23 Swahili Union Version (SUV)

19. Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.

20. Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.

21. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;Na wao waupendao watakula matunda yake.

22. Apataye mke apata kitu chema;Naye ajipatia kibali kwa BWANA.

23. Maskini hutumia maombi;Bali tajiri hujibu kwa ukali.

Mit. 18