19. Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
20. Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.
21. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;Na wao waupendao watakula matunda yake.
22. Apataye mke apata kitu chema;Naye ajipatia kibali kwa BWANA.
23. Maskini hutumia maombi;Bali tajiri hujibu kwa ukali.