13. Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.
14. Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
15. Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
16. Zawadi ya mtu humpatia nafasi;Humleta mbele ya watu wakuu.
17. Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
18. Kura hukomesha mashindano;Hukata maneno ya wakuu.
19. Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
20. Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;Atashiba mazao ya midomo yake.
21. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;Na wao waupendao watakula matunda yake.
22. Apataye mke apata kitu chema;Naye ajipatia kibali kwa BWANA.