3. Kalibuni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Bali BWANA huijaribu mioyo.
4. Mtenda mabaya husikiliza midomo ya uovu;Na mwongo hutega sikio lake kusikiliza ulimi wa madhara.
5. Amdhihakiye maskini humsuta Muumba wake;Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.
6. Wana wa wana ndio taji ya wazee,Na utukufu wa watoto ni baba zao.
7. Maneno mazuri hayapendezi kinywani mwa mpumbavu;Siuze midomo ya uongo kinywani mwa mkuu.
8. Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;Kila kigeukapo hufanikiwa.
9. Afunikaye kosa hutafuta kupendwa;Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.