24. Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu;Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia.
25. Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye,Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.
26. Tena kumwadhibu mwenye haki si vizuri;Wala si kwema kuwapiga wakuu kwa unyofu wao.
27. Azuiaye maneno yake ni mwenye maarifa;Na mwenye roho ya utulivu ana busara.